Wanawake wanaofanya biashara ya kuuza miili na wanaume wanaofanya 
mapenzi ya jinsia moja sasa wanatumia dawa za kufubaza makali ya Virusi 
vya Ukimwi aina ya Truvada kwa ajili ya kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo
 badala ya kutumia mipira ya kondomu. Picha na Maktaba
Kwa ufupi
Mwananchi lilizungumza na baadhi ya wafanyabiashara 
ya ngono jijini katika maeneo ya Mwananyamala Hospitali, Komakoma na 
Vingunguti ambao walisema kuwa wanatumia dawa hizo kwa ajili ya kuzuia 
maambukizi ya VVU ili kuwaridhisha wateja wasiopendelea mipira hiyo.
Habari Kamili
Dar es Salaam. Wanawake wanaofanya biashara ya kuuza miili na wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja sasa wanatumia dawa za kufubaza makali ya Virusi vya Ukimwi aina ya Truvada kwa ajili ya kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo badala ya kutumia mipira ya kondomu.
Dar es Salaam. Wanawake wanaofanya biashara ya kuuza miili na wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja sasa wanatumia dawa za kufubaza makali ya Virusi vya Ukimwi aina ya Truvada kwa ajili ya kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo badala ya kutumia mipira ya kondomu.
Mwananchi lilizungumza na baadhi ya 
wafanyabiashara ya ngono jijini katika maeneo ya Mwananyamala Hospitali,
 Komakoma na Vingunguti ambao walisema kuwa wanatumia dawa hizo kwa 
ajili ya kuzuia maambukizi ya VVU ili kuwaridhisha wateja wasiopendelea 
mipira hiyo.
Baadhi ya wafanyabiashara hao walidai kuwa 
wanatumia Truvada kuzuia maambukizi pindi wanapokutana na wanaume 
wakware ambao huwabaka au kuwalazimisha kufanya mapenzi bila kinga.
“Hizi dawa tunazipata katika hospitali na wakati 
mwingine katika maduka makubwa ya dawa. Kwa sababu zinazuia maambukizi 
ya Ukimwi na sisi ni watu ambao tunafanya kazi katika mazingira 
hatarishi,” anasema Leyla Musa, mmoja wa wanawake hao.
Si hivyo tu, kwa kuwa hii ni biashara baadhi yao 
hukubali kufanya mapenzi bila mipira ili kupata fedha nyingi kutoka kwa 
wanaume.
Wengine hukimbilia huduma ya PEP 
Baadhi ya wanawake hao wanasema kuwa baada ya 
kufanya mapenzi na wanaume kadhaa asubuhi huenda katika kliniki 
zinazotoa huduma za ARV na kudanganya kuwa wamebakwa na kisha hupewa 
huduma za dharura za ARV zinazoitwa kwa kitaalamu Post-exposure 
prophylaxis.
Kwa kawaida mtu aliyebakwa au kujikata hupewa dawa aina ya Lamivudine, Zerophidine au Truvada kulingana na uzito wa tatizo.
“Tunatumia hizi dawa mara kwa mara lakini 
tunafanya hivyo katika kliniki tofauti ili tusigundulike,” alisema mmoja
 wao, mkazi wa Mwananyamala, Mariam Leshaniki.
Kwa maelezo ya Dk Rachel Baggaley, mtaalamu wa 
masuala ya Ukimwi wa Shirika la Afya Duniani anasema dawa za PEP zipo 
maeneo mengi duniani kwa sasa na zinafanya kazi kwa ufanisi pia hazina 
madhara kwa mwanamke.
“Dawa hizi siyo sumu mwilini, zinaingia kwenye 
mfumo wako wa damu kabla virusi havijajizatiti na inavizuia ili mradi 
uzitumie ndani ya saa 72,” anasema Dk Baggaley.
Dawa ya Truvada, ambayo ina mchanganyiko wa dawa 
aina ya Tenovofir na Emtricitabine, imethibitishwa kuwa salama kwa 
kupunguza makali ya VVU pia kuzuia maambukizi mapya. Dawa hizi 
zinazotengenezwa nchini India, zimekuwa msaada mkubwa wa tiba kwenye 
nchi zinazoendelea.
