Serengema ndio sehemu iliyoathirika vibaya zaidi.

Kuna mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi pamoja na chama cha Tanzania Albino katika kuhamasisha na pia kujenga makaazi.

Mashirika yasiyo ya kiserikali yanaamini kuwa uhamasisho na kuacha imani potovu zinaweza kusimamisha mauaji haya. 
 
Mwakilishi wa chama cha Serengema Mashaka Benedict anasema kuwa watu bado wanaamini kuwa sehemu za mwili wa albino zinaweza kuleta utajiri.''Kama hiyo ndiyo hali,mbona sisi si matajiri?''anauliza.

Anadai kuwa watu mashuhuri wanahusika katika ''biashara ya mauaji'' na ndio maanake watu wachache sana wamekamatwa,kushitakiwa,kupatikana na hatia ama kufungwa.''Itakuwa vipi masikini kutoa dola 10,000 kwa kipande cha mwili?,ni wanabiashara na wanasiasa ndio wanaohusika.''

Hata hivyo polisi wanasema kuwa wanachungunza kila moja ya visa lakini wanakosa ushahidi wa kuthibitisha madai yanayotolewa.Kamanda wa polisi wa Mwanza,Valentino Mlolowa anasema,''Kesi hizi ni ngumu kwa kuwa visa hufanyika mashinani sana katika sehemu ambazo hazina stima kwa mfano,na hiyo inafanya kuwajua wahalifu usiku kuwa vigumu.Tunachunguza kila moja ya kesi na madai,lakini kama uonavyo,si rahisi.''

Yaweza onekana kama kuwa tumepoteza kila kitu lakini hii haiwazuilii watu wanaoishi na hali ya Uhalbino kama May Mosi,kutokuwa na tumaini kuwa fedha zinazochangishwa kutoka kwenye kampeni iliyoanzishwa na serikali zitasaidia kusikizwa zaidi kwa Albino nchini Tanzania. 
 Cdt: BBC



 
Top