Furaha ni kawaida yangu, kununa si busara kwangu, kuishi nawewe vizuri ni sehemu ya Maisha yangu, kukusalimia ni hulka ya Moyo wangu, Uhali gani mpenzi?

Uchungu wa kifo hauna tofauti na maumivu nitakayoyapata ukiniachana, mpenzi usiniache nami siko tayari  kukuacha.
Salamu yako ni nusu ya uhai wangu, kuikosa nisawa na kuidhulumu nafsi yangu, kuipata nisawa na ua ridi machoni mwangu, nakila ninapoipata huwa najisikia faraja moyoni mwangu, Nakupenda sana Muhibu wangu.

Mpenzi unawafahamu maadui wa mapenzi yetu ? Ni wale rafiki zako wanaokuletea maneno ya uongo, 
    ndugu zako wanaotugombanisha na wachawi wanotuotea mabaya, tujihadhari tusiwape ushindi. Mapenzi 
    yetu yadumu daima.

 Nakupenda sana P tafadhari usinikasirikie, nimekukumbuka nahitaji kukuona unipoze moyo wangu, 
      njooo mwandani wangu nakusubiri daktari wangu.

Nakupenda sana mwandani wangu ndiyo maana moyo wangu hupatwa kidonda ninaokuona na mwingine 
hasa anapokuwa hana sifa, nahisi kama anakutumia wewe kama mdori wake wa kumfurahisha. Uwe makini ua la moyo wangu.

Mpenzi wangu kukutana nawe ilikuwa ni bahati, kukuchagua kuwa rafiki yangu ilikuwa ni maamuzi yangu, lakini kuanguka kwenye penzi lako haikuwa hiyari yangu. Umeniteka moyo na akili yangu pia.

 Usiku wa leo uwe ni wenye faraja kwako, utawaliwe na usingizi wa mahaba kwenye kope zako, 
      naomba ujenge taswira yangu katika mawazo yako, Usisahau kuniota sweet wangu. USIKU MWEMA

Fungua macho yako uone kopa za mahaba ninazokumwagia, fungua mikono yako na upokee mapenzi yangu, fungua simu yako uone ni jinsi gani ninavyokukumbuka japo kwa kukutumia sms mpenzi wangu, Nakutakia usiku mwema

Utamu wako ni zaidi ya asali, ni wa asili usiohitaji kuongezewa ladha ya sukari, nitaumiss endapo kama ukiwa mbali "NIACHE NIKUPENDE SWEET"

Naweza kukuazima mabega yangu upande, masikio yangu usikilizie mikono yangu ushikie, miguu yangu, utembelee, lakini si moyo wangu kwani tayari unao wewe.

Moyo wangu umehifadhi hisia zako, nakuahidi kamwe sintopunguza upendo kwako, tunza sms hii ya ahadi kwenye simu yako, iwe kumbukumbu kila uisomapo! "NAKUPENDA MALAIKA WANGU"

Si vibaya mimi kukusifia kwani wewe ni wangu, nivingi umejaaliwa, vinavyouvutia moyo wangu, ama hakika uzuri wako umedhibiti matamanio yangu "SINTOMPENDA MWINGINE ZAIDI YAKO"

Thamani ya Mapenzi yako nikubwa kwangu, haifanani nachochote kwenye huu ulimwengu, sina budi kumshukuru mungu, kwa kunijaalia mpenzi mwema unaejali hisia zangu, USICHOKE KUNIPENDA MPENZI

 Kama ungekuwa kidonda kwenye moyo wangu, ningekiacha na maumivu yake ndani yangu.

:Mpenzi kila tunapokuwa chumbani huwa napenda kuwa mbunifu, huwa najitahidi kuepuka udhaifu, ili mapenzi yangu yasikukifu, ENDELEA KUFURAHIA MAPENZI YANGU. Mchana mwema

Wewe ni wapekee ninaekupenda, sifikirii kukusaliti na wala sina wazo la kukutenda, nakuomba tuendelee kupendana siku zote habbity wangu

:Mapenzi ni matamu napia yana raha, wewe hauni ishi hamu, siku zote wanipa raha, wewe kwangu ni mtu muhimu, unaeng'aa moyoni mwangu kama nyota ya jaha. "NAKUOMBA USINIACHE MPENZI WANGU"

 Watu waliniambia ninaweza kufanya chochote kama tu nitaweka mawazo yangu juu ya hicho kitu. Lakini kila nikijitahidi unaipoteza akili yangu

Pokea sms yangu iliyojaa utamu, nimeipamba kwa maneno laini yenye ladha adimu, utamu wake ni kama apple haufanani na ndimu, nimeituma kwako sms hii ikuletee salamu "UHALI GANI MPENZI?"

Dhamira kuu ya Moyo wangu ni Mapenzi, kukupenda kwa dhati bila kipingamizi, kuishi nawewe kihalali kwa kudra za wazazi, Nipende nikupende Tudumishe Mapenzi. "NAKUTAKIA MCHANA MWEMA MPENZI WANGU"au ahsubui nk
 
Top