Viongozi wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Mkoani Rukwa wameamua kuachia ngazi kwa kujiuzuru, ambapo mwenyekiti wa chama hicho na katibu wa mkoa huo pamoja na baraza zima la uongozi la mkoa wametangaza kuwa watabaki kuwa wanachama wa kawaida, kwa kile
walichokidai kutoridhishwa na maamuzi ya makao makuu katika uteuzi wa nafasi ya
ubunge wa viti maalumu kupitia chama hicho.

Kwa upande wake katibu wa
Chadema wa mkoa wa Rukwa Bw Ozem Chapita, akitoa ufafanuzi wa hatua hiyo
amesema uteuzi wa mtu ambaye anaonekana ni msaliti, kunaweza kukaathiri hata
uwezekano wa chama hicho kilichoshinda viti kumi kati ya tisa vya udiwani, kuweza
kuiendesha halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga kwa kuwa na meya wa manispaa,
kwa kushindwa kupata kura za kutosha.