Picha: Sehemu Za Binadamu zilizoathirika na Magonjwa ya Ngono

NINI KIJANA ANAPASWA KUJUA KUHUSU MAGONJWA YA NGONO?
Magonjwa ya Ngono ni magonjwa yanayoambukizwa kwa tendo la kujamiiana na mtu aliyeambukizwa magonjwa hayo bila kutumia Kondomu. Magonjwa haya huweza kuwapata watu wa rika zote hususani wale walio katika umri wa kuzaa (Kati ya miaka 15 - 49)

Vijana walio katika umri kati ya miaka 10 hadi 24 wanawakilisha 1/3 ya idadi ya wakazi wote wa Tanzania. Kundi hili liko katika hatari zaidi ya maambukizi ya magonjwa ya Ngono kwakuwa wanapobalehe wanapata hisia za kupenda na pia hamu ya kufanya tendo la kujamiiana kujitokeza kwa nguvu

Hali hii huchochewa na Vichocheo/Homoni vilivyomo mwilini ambavyo katika kupanda katika kupanda na kushuka husababisha hisia za kufanya tendo la Kujamiiana.

Hivyo basi ikiwa watakosa Ufahamu wa Kutosha Kuhusu miili yao wanaweza kujiingiza katika tabia Hatarishi za Kujamiiana bila Kondomu na mwenzi zaidi ya Mmoja.
Read More>>













 
Top