MAHUSIANO YA DAWA ZA KULEVYA NA VVU/UKIMWI UKOJE?
Matumizi ya sawa za kulevya yanaongezeka nchini na hivyo kuchangia kuleta madhara makubwa katika jamii yetu. Moja ya madhara hayo ni kuenea kwa VVU miongoni mwa watumiaji wa madawa hayo, wenzi wao na hata kusambaa kwenye jamii yote.

Matimizi ya madawa ya kulevya kwa wale wenye maambukizi ya VVU huongeza kasi ya kupatwa na ukosefu wa Kinga Mwilini (UKIMWI) na hivyo kuambukizwa magonjwa nyemelezi kirahisi zaidi na kufa mapema.
  Muathirika wa Madawa Ya Kulevya na VVU

DAWA ZA KULEVYA ZINAWEZAJE KUENEZA VIRUSI VYA UKIMWI?
matumizi ya madawa ya kulevya huweza kueneza VVU kwa namna mbili tofauti:
  • Kufanya ngono sizizo salama baada ya uwezi wa kufikiri na kutoa maamuzi kwa mtumiaji kuathirika na dawa hizo.
  • Kushirikia na sindano au mabomba au vifaa vingine vya kujidungia wakati wa kuzitumia dawa hizo.
Wakati vitendo hivi huwaweka watuiaji wa dawa za kulevya katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU na hata kuwaambukiza wengine. Tafiti zinaonesha kuwa:
  • Mwaka 2004, 31.3% ya wanaojidunga kutoka katika jiji la Dar es salaa waliambukizwa VVU
  • Maambukzi ya VVU miongni mwa wanaojidunga katika jiji la Dar es salaam yalifikia 42% mwaka 2006.
Kijana akijidunga sindano yenye dawa za kulevya
 
Zifahamu Tabia Hatarishi kwa Vijana
Soma hapa>> 

________________________________________________________________________________



________________________________________________________________________________
  • Sababu Zinazopelekea Vijana Kupia mande/Mtungo Read More>>
________________________________________________________________________________
 
Top