Kutokana na tathmini ambayo imefanywa na wataalamu mbalimbali imebainika kuwa ni asilimia 25 tu ya wanawake ambao wanafika kileleni wakati wa kufanya mapenzi ama tendo la ndoa hapa ulimwenguni. Hali hii huweza kusababishwa na mambo mbali mbali kama yafuatayo:

1: Afya ya mwanamke. Ili binadamu yeyote aweze kufurahia tendo la ndoa ni lazima awe na afya nzuri. Inakuwa ni kitu kigumu sana kwa mwanamke kuweza kufika safari ya mapenzi endapo afya yake haikubaliani na ubongo. Hivyo magonjwa huweza kusababisha mtu hasa mwanamke kwa namna moja ama nyingine kutokufurahia tendo. Kitu cha kufanya ni kuhakikisha mpenzi wako anafanyiwa uchunguzi wa kibailolojia na kupatiwa matibabu haraka sana ikibainika kuwa ni mgonjwa.

2. Jambo la pili ambalo mwanamke ama mtu yeyote anatakiwa kulizingatia ni utayari katika kufanya tendo la ndoa. Endapo Mwanamke hayupo tayari kufanya tendo hilo ni vigumu kufurahia shughuli na badala yake mtu wa namna hiyo huambulia maumivu kuanzia mwanzo hadi mwisho wa shughuli. Hali hii hutokea kwasababu kuna uhusiano mkubwa sana wa ubongo na hisia za kimapenzi. Endapo utakumbana na hali kama hiyo unatakiwa kufanya kila namna ambayo mwenzi wako atakuwa tayari kisaikolojia na kimwili kufanya shughuli husika.
3. Jambo lingine ambalo huambatana na hili ni hali ya uchovu. Hili nalo huweza kusababishwa na mizunguuko mingi ama kufanya kazi nzito ambazo humchosha mwanamke na kumsababishia akili yake kuchoka pia. Endapo mwanamke atakuwa amechoka ni vigumu sana kwa kumfanya afurahie tendo.  Hali hii si kwa mwanamke tu bali hata kwa mwanaume pia. Kwahiyo jambo la kufanya ili kuepuka tatizo hili ni kuhakikisha mwanamke amepumzika vya kutosha kabla ya kuanza shughuli.

4. Mazingira yanaweza kusababisha mwanamke asifike safari yake. Kujirudia kwa mazingira ya kufanyia shughuli mara kwa mara huweza kusababisha mtu kushindwa kufikia safari yake. Imezoeleka kuwa eneo pekee ambalo kwa kawaida hufaa zaidi kufanyia mahandosi ndi chumbani tena kitandani pekee. Hali hii huweza kumfanya mwanamke kuzoea mazingira na kuyachoka pia. Kwa namna hiyo ni vyema kujitahidi kubadilisha mazingira. Kwamfano kama mmezoea kukutana chumbani basi siku nyingine mahandosi yanaweza kuendelea hata jikoni, bafuni, ama sitingrum. Ilimradi mazingira yamebadilika. Vilevile inaweza kuwa ni chumbani lakini isiwe kitandani kama ilivyo mazoea yenu. Pia unaweza kubadili hata aina ya taa kama ni usiku, unaweza kutumia taa ya rangi badala ya taa yenye mwanga mkali. Endapo umezoea kutumia chemli basi unaweza kutumia hata kibatari ama mshumaa.  Pia harufu ya manukato ambayo yanampendeza mwenzi wako yanaweza kuvuta hisia zaidi na kumfanya kuwa tayari.

5. Kukosekana kwa maandalizi ya kihisia kabla ya tendo. Hili ni jambo la msingi sana ambalo linampasa mwanaume yeyote kulifahamu kabla ya kukutana na mpenzi wake. Kwa mkulima ni lazima kuandaa shamba kabla ya kupanda, kwa mvuvi ni lazima kuandaa nyavu zake kabla ya kuingia majini, na kwa muwindani ni lazima kuandaa silaha zake kabla ya kuingia mawindoni, Halka dhalka kwa mpenzi ni lazima kumuandaa mwenzi wake kabla ya kuanza shughuli ya kuserebuka.

6. Mwanaume kuwahi kufika kileleni kabla ya mwanamke. Katika hili napenda kuweka wazi kuwa wanawake ni tofauti na wanaume. Wanawake walio wengi huchukua muda mrefu zaidi kuweza kufika mwisho wa safari. Kwa utafiti iliyofanyika na wataalamu wengi Imebainika kuwa wanawake walio wengi wanaweza kufika safari ya mahabati kuanzia dakika 45 hadi 60 na kuendelea. Kutokana na hali hiyo wanawake wa namna hiyo wanajikuta wakiwa katika bahati mbaya siku zote hasa wanapokutana na wanaume ambao wanapiga bao kila baada ya dakika 10 ama 15.

7. Mwanamke kukosa maandalizi ya kutosha kabla ya tendo. Naomba hapa tuelewane kidogo, wanawake hutofautiana kutoka mmoja na mwingine. Wapo ambao huwa hawachelewi kufika safarini (Mshindo), na wakati mwingine utakuta wakati wa maandalizi tu wenyewe anakuwa wamekwisha jisevia mara kadhaa na pindi unapoingia kwenye shughulini unakuwa unamtafutia safari nyingine. Halka dhalka kuna wanawake wengine si rahisi kuweza kuwapata katiaka wakati wa maandalizi hasa kama utashindwa kufahamu maeneo nyeti ambayo huweza kumletea mshawasha na hamasa ya shughuli. Endapo mwanaume utakuwa umefanikiwa katika kipindi hiki basi hautapita muda mrefu kuweza kumpeleka mwenzio pale panapostahili.  

Kuzoea staili/ mikao ya kufanya mapenzi. Suala jingine ambalo ni nyeti katika tendo la ndoa ni matumizi ya staili. Watu walio wengi hasa waafrika wamezoea staili moja tu ya kifo cha mende, naweza kusema staili hii ni maarufu sana. Inaaminika kila mtu ambaye amewahi kushiriki katika shughuli hii basi amewahi kuitumia staili hii. 
Kwahiyo Endapo kila unapokutana na Mchuchu mkao (Staili) inayotumika ni ileile ya kila siku, Lazima kuwepo na ugumu kwa mwanamke huyo kuweza kufikia safari yake akiwa salama. Hali hii inamfanya kukuzoea na kukuona yuleyule na hatimaye kukuchoka. Lakini kama unakuwa ukimbadilishia staili kila mnapokutana, atakuona mpya kila kukicha hata mkiishi kwa miaka zaidi ya miamoja. Unaweza kutumia staili kama vile Mtwike, mwendochatu, mwitemwima, kitakobega,mkondonungwi, nk



 
Top