Basi la kampuni ya Morobest Scania yenye namba za usajili T258 AVH limepata ajali asubuhi ya siku ya Jumatano baada ya kugongana usokwa uso na Lori maeneo ya Kongwa mkoani Dodoma.
Katika ajali hiyo imeripotiwa kuwa watu 17 walipoteza maisha hapohapo na wengine 56 kujeruhiwa vibaya.


Kamanda wa Polisi Mkoani Dodoma amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na amesema kuwa chanzo chake ni uzembe wa madereva (Dereva wa Lori) ambapo dereva wa Lori ambaye kwa sasa ni marehemu alikuwa akijaribu kulipita Lori jingine kabla ya kukutana uso kwa uso na basi hilo la Morobest na kusababisha vifo vya watu hao na majeruhi.

Marehemu ambao walitambuliwa katika ajali hiyo ni pamoja na 

Dereva wa lori Gabriel Lemanya Mkazi wa Ndebwe wilayani Chamwino,
Dereva wa basi Said Lusogo,
kondakta wa basi Omari Mkubwana,
Mikdadi Zuberi ambaye alikuwa ni utingo wa Lori.

Wengine ni
Justin Makasi, Gabriel Chiwipe, Marick Masawe, Melina Maliseli, Wilson Sudai wote wakazi wa Mpwapwa na watu wawili waliotambulika kwa jina moja moja ambao ni Christina mkazi wa Mpwapwa na Nasibu mkazi wa Kongwa.


    



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjYvm_XcCTOmnLr13aNB3BT_-ugnjCaPHXrkeVqqahEK5Yov_uklI0KcFZI0hwpZw9TPzxOk7FWiiN6C_QV-yMLS9rVRrpWXdM-EHNjs9hETk2YaMTL8EwsGVQ0u-Fw0HbuZJjsduWchJU/s1600/IMG-20140730-WA0008.jpg Miili ya marehemu wote imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Kongwa na wengine katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma, huku majeruhi nao wakilazwa katika hospitali hizo kwa matibabu.
 
Top