Tunapo sema tatizo la kufika kileleni tunazungumzia makundi makuu matatu, ambayo ni Kuwahi kufika kileleni kwa muda mfupi mno, kuchelewa kufika kileleni, na kufika kileleni kusiko sawa. Matatizo yote haya tunayaelezea hapa chini moja baada ya jingine.

1.    KUCHELEWA KUFIKA KILELENI

Mwanaume ambaye anatatizo kama hili huwa anachukua muda mrefu sana kufika kieleni wakati anapofanya mapenzi, au wakati mwingine kushindwa kabisa kufika kileleni hata kama awe anapenda na anapata hisia katika kufanya mapenzi. Tatizo hili kitaalamu huitwa Retarded ejaculation

Matibabu yaliyopendekezwa kitaalamu kupatiwa mtu mwenye tatizo hili la kuchelewa kufika kileleni yanatakiwa yaendane na sababu ya tatizo lenyewe. Kama inadhaniwa kuwa chanzo chake ni athari za kutumia dawa Fulani (side effect), kubadilisha dozi na kutumia nyingine kutasaidia kuondoa tatizo hilo. Lakini kama tatizo linaaminika kuwa limesababishwa na athari za kisaikolojia, inatakiwa kupewa ushauri wa kisaikolojia.
Wanaume walio wengi hawahitaji kupatiwa huduma ya matibabu ya tatizo la kuchelewa kufika kileleni kwasababu bado wanao uwezo wa kufurahia tendo la ndoa, na pia hali hii haina madhara kiafya. Ingawa yapo matibabu yanayo wezakuondoa tatizo na kumfanya mhusika kufika kileleni.
Hata hivyo kama unahitaji kuwa na watoto na kuitwa baba basi upo ulazima wa kufanyiwa matibabu haraka. 

2.    KUFIKA KILELENI KUSIKO KWA KAWAIDA

Aina hii ya tatizo linatokea wakati mwanaume anapofika kileleni mbegu za kiume/shahawa zinarudi nyuma na kuingia kwenye kibofu cha mkojo badala ya kuelekea kwenye mirija ya kutolea shahawa hizo nje.
Mwanaume mwenye tatizo hili huwa anapofika kileleni anajisikia raha kama wengine lakini yeye mbegu zake hazitoki nje, na kama zikitoka basi huwa ni chache mno.
Tatizo hili halina madhara yoyote ya kiafya kwa mwenye nalo, isipokuwa linaweza kumletea ugumba wa mwanaume na kushindwa kupata mtoto. (Kitaalamu tatizo hili huitwa Retrograde ejaculation

3. TATIZO LA KUWAHI KUFIKA KILELENI

Kitu cha kwanza kabisa ambacho ningependa kukiweka wazi kwako ni kwamba tatizo hili la kuwahi kufika kileleni ni janga la kidunia, ambapo mwanaume anajikuta akifika kileleni mapema sana wakati wa kufanya mapenzi kinyume na kupenda kwake.
Wanaume wengi hawaelewi ni muda gani ambao ni wa kawaida wanatakiwa kufika kileleni wakati wanapokutana na wapenzi wao. Wataalamu waliobobea katika masuala haya wamefanya uchunguzi wao kwa kutumia wanaume 500 kutoka katika nchi tano (5) tofauti za hapa ulimwenguni. Umepatikana wastani wa muda ambao hutumiwa na wanaume kufika kileleni mara tu wanapoingiza uume wao kwenye uke wa wapenzi wao ni kati ya nusu dakika na dakika tano.
Ingawa ni jukumu la mtu na mpenzi wake kukaa na kujadili wenyewe kama endapo wanaridhika ama hawaridhiki kutokana na muda ambao mwanaume anautumia kufika kileleni, Kwakawaida kufika kileleni kabla ya dakika ama ndani ya dakika moja mara tu mwanaume anapoingiza uume wake kwenye uke wa mwenziwake, linachukuliwa ni kama tatizo la na linahitaji kupatiwa ufumbuzi mapema.

Mambo ambayo yanaweza kusababisha tatizo hili la kufika kileleni ni,


·  Msongo wa mawazo, 

·  Migogoro katika mahusiano,

·  Mama ulishawahi kupata shida yoyote katika mapenzi siku za awali, 

·  Kutokuwa na furaha, 

·  Magonjwa kama vile kwashakoo na mengineyo. 

·  Baadhi ya wataalamu waliofanya uchunguzi wanadhani kuwa baadhi ya wanaume wanakabiliwa na tatizo hili kutokana na maumbile yao, kama vile kuwa na uume ambao hauna nguvu (Kuzaliwa Hanithi) 

·  Kufika kileleni kusiko kwa kawaida kunasababishwa na kuharibika kwa mishipa au misuri ambayo inazunguuka kwenye shingo ya kibofu cha mkojo. Uharibifu huu unaweza kusababishwa na kufanyiwa upasuaji wa kibofu cha mkojo


 
Top