Mahabusu wa Gereza la Biharamulo mkoani Kagera wamefanya mgomo baada ya kusota kwa miaka mitatu ndani pasipo kusikilizwa mashauri yao.



Ameeleza mtoa habari wetu kuwa Mahabusu wa Gereza hilo wanaotuhumiwa kuwa na kesi za mauaji wameamua kuchukua jukumu hilo wakiamini kuwa ni njia itakayoweza kuwashinikiza mahakama Kusikiliza kesi zao ambazo nyingine ni za zaidi ya miaka mitatu.



Baada ya kupata Habari hiyo Utamu war aha ilifanya jitihada za kumtafuta mkuuwa gereza hilo ili kuzungumzia suala hilo lakini haikufanikiwa kwa simu yake kutokupatikana.
 
Top