Mtu mmoja ambaye hakuweza kufahamika jina lake amefariki dunia baada ya kugongwa na treni ns kuburuzwa umbali wa mita mia maeneo ya Kinguruwila mjini Morogoro.
Mwanahabari wetu akishuhudia tukio hili amesema kuwa viungo vya mwili wa mtu huyo ambavyo vimetapakaa umbali huo wa mita mia kama vile miguu, mikono, na kifua vimeokotwa lakini kichwa hakikuweza kupatikana na hakijulikani kilipo.
Wananchi wa eneo hilo wamsema kuwa inawezekana mtu huyo alikuwa maelewa na kushindwa kuepukana na ajali hiyo.
Kamanda wa reli Enginea Simon Chillery
akizungumza kwa njia ya simu akiwa njiani kuelekea nachingwea
amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo na amesema mtu huyo ambaye
hakufahamika jina lake anakadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 35 na 40
na uchunguzi wa tukio hilo unaendelea na kuwakumbusha wananchi
kuheshimu sheria za reli kama ilivyo sheria za barabarani kwa watembea
kwa miguu na wanaendesha vyombo vya moto wanapovuka reli