Akizungumzia utafiti huo mhadhiri wa Uhandisi wa Mazingira kutoka Chuo kikuu cha Ardhi ‘Aru’ Willium Mwagoha alisema  waligundua mabwawa ya majitaka yanayotoka mabibo, dampo la vingunguti, viwandani na gereji mbalimbali yanamwaga maji kwenye mto huo.


Dk.Mwegoha alisema mboga zilizomwagiwa maji hayo zilibainika kuwa na sumu zilizokuwa na madini ya risasi,shaba na kromiamu ambazo zote zina madhara kwa binadamu.


Aliasema katika utafiti huo walibaini kuwa mboga hizo zinauzwa kwenye masoko ya Ilala, Kariakoo, Buguruni, Veterani,Tazara, Mwananyamala, Mnyamani, Kigogo, Kisutu, Vingunguti, Tabata, Mikoroshini na maeneo ya jirani na wkaulima hao.

Crdt: Nipashe 






 
Top