Wakazi wa jiji la Dar es salaam wapo
katika hatari ya kupatwa na magonjwa makubwa kamasaratani, utasa, kupoteza
uwezo wa kuona,kuharibu ubongo,maini na figo kutokana na matumizi ya mboga
za majani zinazolimwa katika mabonde ya jiji hilo.
Matumizi ya mboga hizo ni makubwa
jijini humo,yakitokana na umuhimu wake kwa afya za watu na hali duni ya
maisha inazozifanya familia nyingi kumudu gharama zake ikilinganishwa na
vitoweo vingine.
Sehemu kubwa ya mboga hizo inatokana
na kilimo kinachofanyika katika mbonde la mto Msimbazi namaeneo ya
Kigogo-Sambusa,Ubungo,Gereji mchicha,Vingunguti na Tandale.
Katika Gazeti la NIPASHE limesema tayari matokeo
ya tafiti kadhaa yamedhihirisha maji yanayotumika kwa umwagiliaji wa
mboga za majani jijini humo kuwa na kemikali zenye sumu ama taka zinazotoka
viwandani na kwenye makazi ya watu.
Pili wakazi wanaoishi pembezoni mwa
bonde la Msimbazi na maeneo mengine yanayolimwa mboga hizo,wamebainika kutupa
taka kama betri zilizoisha muda wa matumizi,masalia ya simu za mkononi,vipuri
vya magari na majokofu mabovu.
Taka hizo zenye sumu zinatupwa
kwenye mifereji ya maji yanayotumika kwa umwagiliaji wa mboga hivyo kuzidi
kuhatarisha afya za walaji.
Chuo Kikuu cha Ardhi kilifanya
utafiti katika bonde la mto Msimbazi na udongo na maji kwa vigezo vya Shirika
la Afya dunia WHO na Shirika la viwango nchini TBS. Endelea>>