Marehemu waliotambulika kwa majina ni wanne ambao ni 1. Thomas Simfukwe (35) 2. Exavery Mumbisa (34) 3. Amina Maiko (30) 4. Neema Almasi 5. Hebeli Mkilimi 6. Rose Hezron Halele na 7. aliyefahamika kwa jina moja Januari.

 Watu tisa [09] kati yao wanaume saba [07] na wanawake wawili [02] wamefariki dunia baada ya gari waliokuwa wakisafiria lenye namba za usajili T.203 ARZ aina ya Toyota Coaster lililokuwa likiendeshwa na dereva aitwaye John Emanuel (36) mkazi wa mlowo-mbozi likiwa linatokea Mbeya kwenda Tunduma wakati akijaribu kulipita gari T.789 AZL/T.123 AXY aina ya Tata Truck eneo ambalo kuna mlima na mbele yake kuna kona lilitokea gari T.903 CVF aina ya Tata basi hivyo dereva wa coaster kulazimika  kuingia mbele ya lori  alilokuwa analipita na kugongwa ubavuni upande wa kushoto pia kugongwa upande wa kulia na basi aina ya Tata tajwa hapo juu.


Tukio hilo limetokea mnamo tarehe 21.12.2014 majira ya saa 14:10 mchana huko katika kijiji cha Chengula, kata na tarafa ya Tunduma, wilaya ya Momba, mkoa wa Mbeya, barabara kuu ya Mbeya/Tunduma. 

Marehemu waliotambulika kwa majina ni wanne ambao ni 1. Thomas Simfukwe (35) 2. Exavery Mumbisa (34) 3. Amina Maiko (30) 4. Neema Almasi 5. Hebeli Mkilimi 6. Rose Hezron Halele na 7. aliyefahamika kwa jina moja Januari.

Hata hivyo miili ya marehemu watatu bado kutambuliwa. Aidha katika ajali hiyo watu kumi na moja [11] walijeruhiwa ambao majeruhi sita [06] wanaume, wanne [04] wanawake, wawili wamelazwa katika hospitali ya rufaa Mbeya ambao ni dereva aitwaye John Emmanuel Mzumba (36) mkazi wa Mlowo na kondakta aitwaye Christian Mtende (31) mkazi wa Mlowo na wengine saba walipelekwa katika hospitali ya serikali wilaya ya Mbozi na kituo cha afya Tunduma kwa matibabu. 

Chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa toyota coaster kutaka kuyapita magari yaliyokuwa mbele yake bila kuchukua tahadhari.

Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi Ahmed z. Msangi anatoa wito kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto ikiwa ni pamoja na kuzingatia sheria na alama za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoepukika.


 

 Hii ndio coaster iliyotoa roho za ndugu zetu maeneo ya sogea mlima chengula tunduma


 
Top