
Tukio la kusikitisha limetokea
katika nchi ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo likiwaonesha wanajeshi kwa
kushirikiana na wananchi wenye hasira kali kumuua kwa kumpiga vibaya mawe na
vitu vyenye ncha kali kibaka mmoja alieiba begi.
Katika hali ya kushangaza wanajeshi
hao wakiwa wamevalia sare zao za kijeshi walionekana wakijumuika na wananchi
wenye hasira kali kwenye kumuua kibaka huyo, jambo ambalo watu walitegemea kuwa
kwa uwepo wa wanajeshi hao pengine kibaka huyo asingepigwa na badala yake
angeokolewa mikononi kwa raia wenye hasira kali na sheria ingechukua mkondo dhidi
yake, lakini tukio lilienda ndivyo sivyo baada ya wanajeshi nao kuonekana
kumchangia kibaka huyo pamoja na raia kwa kumpiga mpaka kumuua.
Tukio hili ambayo ilizua mzozo
mkubwa nchini humo mpaka kufika kwa mkuu wa majeshi ambapo alisema "tukio
hili ni la kisikitisha pia kulidhalilisha jeshi, hatua kali za kijeshi
zitafuatwa kwa wanajeshi walioonekana kushiriki kwenye tukio hili". Pia
aliendelea kusema wanajeshi hao watatafutwa mpaka wapatikane na hatua kali
zitachukuliwa dhidi yao.
Hata hivyo wananchi wa nchi
hiyo wameonekana kukosa imani na wanajeshi wao, kwani kwa tukio hilo baya
walilolifanya limewaongezea hofu na kusisitiza nidhamu za kijeshi ziongezwe ili
wanajeshi wajue majukumu yao ya nini la kufanya iwapo wataona kuna tukio baya
limetokea katika eneo walilopo.
CRDT: Nyuma ya Pazia
CRDT: Nyuma ya Pazia