Mwili wa Kijana baada ya kuchomwa kisu
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Hamisi Selemani (18) mkazi wa Vingunguti jijini Dar es salaa, amefariki dunia baada ya kuchomwa kisu maeneo ya kifuani kwake.


Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kimeeleza kuwa Hamis ameingia katika mauti hayo baada ya kufumaniwa na msichana anayedaiwa kuwa ni mpenzi wa mtu (Jina limehifadhiwa) mwenye miaka 15. Mtu ambaye anatuhumiwa kutenda tukio hilo amefahamika kwa majina ya Ali Kimondo ambaye ndiye anayedaiwa kuwa mpenzi wa msichana huyo. 


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na ameeleza kuwa, tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia mwaka mpya majira ya saa 9:00 usiku katika eneo la Vingunguti Magenge.


Nzuki aliendelea kueleza kuwa baada ya tukio hilo Ali Kimondo pamoja na msichana huyo walitoroka, kwa namna hiyo Jeshi la polisi linaendelea na upelelezi kwaajili ya kuwapata watuhumiwa hao.
 
Top