Ni jambo linaloweza kuwa geni kidogo kwa baadhi ya makabila, lakini kwa baadhi ya Wachaga wa Kilema mkoani Kilimanjaro kuna mila ambazo kwa makabila na jamii nyingine zinaweza kuwa za kushangaza.
Jamii hii inaonekana kuwa tofauti na Wachaga wengine kwani wao huwafukua wapendwa wao waliofariki kila wanapotimiza miaka minane hadi 10 baada ya kuzikwa.
Mila hiyo ina taratibu zake za kufuata kabla ya kufikia hatua ya mwili kufukuliwa sehemu ulikokuwa umezikwa na kwenda kuhifadhiwa sehemu nyingine.
Kitendo cha kufukua maiti kimekuwa kikifanywa kwa kufuata taratibu maalumu za kimila na zisipofuatwa inaaminika huwa na madhara makubwa kwa ukoo ikiwamo kusababisha kifo.
Mmoja wa wanaukoo wa Lyimo, Edward Lyimo anasema utamaduni huo aliukuta tangu akiwa mdogo na unaendelea mpaka sasa akiwa mtu mzima.
“Si jambo la ajabu. Katika utu uzima wangu nimeshafukua ndugu zangu wengi tu waliokufa miaka ya nyuma na kuihifadhi eneo maalumu lililotengwa na familia kwa ajili hiyo,” anasema.
 
Top