Jeshi la polisi Njombe likitoa kichapo kwa wanafunzi
wa Njombe sekondari school (NJOSS)

Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Njombe (NJOSS) wamejikuta katika wakati mgumu baada ya kuchoma moto shule yao.

Kwa mujibu wa mkuu wa shule hiyo: Mwalimu Benard William amesema kuwa huenda chanzo cha tukio hilo kikaendana na uamuzi uliofanywa na bodi ya shule hiyo ambayo ilikutana Oktoba 7 mwaka huu na kuadhimia kuwasimamisha shule wanafunzi waliokuwa wametoroka shuleni usiku na kwenda Disco. Akamalizia kwa kusema kuwa hata hivyo Uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.

Kamishna wa elimu nchini ameifunga shule ya Njombe (NJOSS) kwa kipindi cha mwezi mmoja kufuatia vurugu hizo zilizopelekea uharibifu mkubwa wa mali zinazokadiriwa kuwa zaidi ya shilingi za kitanzania Milioni moja.

Afisa elimu shule za sekondari mkoani Njombe Said Nyasiro amesema kwa wanafunzi hao wanatakiwa kurejea shuleni hapo baada ya mwezi mmoja wakiwa na wazazi wao pamoja na pesa kiasi cha shilingi Lakimoja na Nusu kila mmoja kwaajili ya kufidia mali zilizoharibika.

Hata hivyo jeshi la polisi mkoani Njombe limefanikiwa kuwashikilia baadhi ya wanafunzi kuhusishwa na chanzo cha vurugu hizo, huku wengine wakisurubiwa vikali, kama wanavyoonekana kwenye picha.
 

 

 

  
Baadhi ya wanafunzi wa Njombe sekondari wakipokea kichapo kutoka kwa Jeshi la polisi



 _________________________________________________________________________________

 
Top