Home
»
» Unlabelled
» ACHINJWA KAMA KUKU BAADA YA KUMCHINJA MWANAE
Tukio lilitokea hivi karibuni mkoani Mara la mama wa
kambo kumchinja mtoto wake kwa kutumia panga hadi kufariki, limechukua sura
mpya baada ya mama huyo nae kushambuliwa na wananchi wenye hasira kali kwa
kukatwa katwa na mapanga mpaka kufariki.
Tukio la kukatwa katwa mapanga mama huyo limetokea baada
ya wananchi wa kijijini hapo walioshikwa na jazba kali kwa kutokubaliana na
kitendo cha kinyama alichomfanyia mtoto huyo kwa kumkatishia maisha yake.
Hata hivyo wananchi walionekana kujichukulia hatua
mikononi kwa kumuua mama huyo, kwa kile kilichodaiwa hawakuona hatua zozote za
kisheria alizochukuliwa mtuhumuwa huyo kwa kitendo cha kinyama
alichokifanya.
Awali mwenyekiti wa kijiji alifatwa na wanakijiji
kuulizwa ni hatua gani ya kisheria mtuhumiwa atachukuliwa kwa mauaji ya kinyama
aliyoyafanya kwamaana baada ya tukio, mtuhumiwa alionekana kutochukuliwa hatua
yeyote ya kisheria kwa muda mrefu licha ya serikali ya kijiji na polisi kupata
taarifa ya kutokea tukio hilo.
Mwenyekiti wa kijiji aliwajibu wanakijiji kuwa polisi
wanatambua kutokea kwa tukio hilo na watakuja kumkamata mtuhumiwa na hatua za
kisheria za mauaju zote zitafata juu yake.
Muda ulizidi kutokomea bila kuonekana dalili zozote za
mtuhumiwa huyo kuchuliwa hatua, ndio wanakijiji wenye hasira kali walipomvamia
mama huyo na kumkatakata kwa mapanga kulipiza kisasi kwa kile alichomfanyia
mtoto wake.
Mwenyekiti wa kijiji analilaumu jeshi la polisi kwa
kuchelewa kumchukua hatua mtuhumuwa mpaka maafa makubwa mengine kutokea.
Picha zikionesha Tukio lilivyoku
SOURCE: Mwanamalunde