Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paul
Mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja mkazi wa kijiji cha Kindo wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro amefariki dunia baada ya kunyongwa na baba yake wa kambo kufuatia migogoro ya kifamilia kati yake na mkewe.


Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paul amesema mtoto Abdallah Hamis amenyongwa na baba yake wa kambo Zamili Shabani (27) muda mfupi baada ya mama wa mtoto kwenda dukani kununua mahitaji na aliporejea aliingia chumbani kumwamsha mtoto ndipo akagundua kuwa mtoto amekufa ambapo mtuhumiwa kwa wasiwasi alianza kukimbia na mama huyo alipiga kelele ya kuomba msaada kwa majirani hadi alipokamatwa.

Mtuhumiwa amekamatwa na atafikishwa mahakamani kwaajili ya kujibu shitaka.

Crdt: Malunde
 
Top