Mahakama moja nchini Uswizi imempiga faini mwanamume mmoja aliyebofya alama ya kupenda au "like" kwa Kiingereza katika maoni yaliyotolewa kwenye ujumbe ulioandikwa katika Facebook.
Ujumbe huo ulikuwa wa kumharibia mtu mwingine sifa.
Kesi hiyo ilihusiana na maoni ambayo yalitolewa kumhusu Erwin Kessler, ambaye ni mkuu wa shirika la kutetea haki za wanyama.
Alidaiwa kuwa mweneza chuki dhidi ya Wayahudi na mbaguzi wa rangi, taarifa kwenye vyombo vya habari zinasema.
Mahakama ya ngazi ya wilaya mjini Zurich ilisema mshtakiwa "bila shaka alionekana kuunga mkono ujumbe huo na kuufanya kama wake" kwa kupenda maoni yaliyokuwa yametolewa.
Kwa mujibu wa gazeti la Le Temps la Uswizi, mwanamume huyo alibofya kitufe cha kupenda katika maoni sita.
Bw Kessler anadaiwa kuwashtaki watu zaidi ya kumi kuhusiana na maoni ambayo yalitolewa kwenye Facebook mwaka 2015.
Waliochangia wanatoa maoni kuhusu mjadala wa iwapo makundi ya kutetea haki za wanyama wanafaa kuruhusiwa kushiriki katika tamasha la wasiokula nyama, gazeti la Tages Anzeiger limeripoti.
Amr Abdelaziz amesema mahakama Uswizi zinahitaji kutoa ufafanuzi kwa watu wanaotumia mitandao ya kijamii na kuonga kwamba uhuru wa kujieleza huenda ukaathiriwa pakubwa iwapo watu watahukumiwa kwa "kupenda" ujumbe kwenye Facebook.
Chanzo: BBC

Habari nyingine:

 MATUKIO ZAIDI YA KUSISIMUA BOFYA HAPA 

AJIRA MPYA ZIMETANGWAZWA, BOFYA HAPA
http://studentswagas.blogspot.com/

 
Top