Mtuhumiwa wa wizi akiwa amechakazwa kwa kipigo
Mashuhuda wa tukio hili walisema kijana huyo na wenzake waliiba pikipiki mbali na hapo Mwembechai ila katika purukushani na wamiliki wa chombo kile, kijana yule alijikuta akianguka kutoka kwenye pikipiki
MKatofari yaliyotumika kumshambulia mtuhumiwa
Wananchi wakiwa katika jaribio la kumvisha tairi mtuhumiwa na kumchoma moto


Mtuhumiwa akibebwa na Polisi


Askari wakiwa eneo la tukio


Gari la Polisi likiwa eneo la tukio


Damu ya Mtuhumiwa ikiwa imetapakaa eneo la tukio


Umati wa wananchi wakishuhudia Tukio


Mtuhumiwa akiwa katika hali mbaya
KIJANA ambaye jina lake haikufahamika mara moja, amenusurika kuuawa na wananchi wenye hasira kwa tuhuma za wizi wa pikipiki jijini Dar.Tukio hilo la kusisimua limetokea asubuhi ya leo Magomeni-Mwembechai,  ambapo lilisababisha foleni ndefu ya  magari wakati kijana huyo akiadhibiwa na wananchi.
Mashuhuda wa tukio hili walisema kijana huyo na wenzake waliiba pikipiki mbali na hapo Mwembechai ila katika purukushani na wamiliki wa chombo kile, kijana yule alijikuta akianguka kutoka kwenye pikipiki eneo lile na kuzingirwa na waendesha pikipiki wa pale wanaojulikana kama ‘bodaboda’ walioanza kumshushia kipigo baada ya mmiliki wa pikipiki husika aliyekuwa akiwafukuza kusema kijana huyo alikuwa na wenzake waliokimbia na chombo hicho.
Pamoja na kipigo alichopewa, wananchi waliamua kumvisha tairi shingoni wakiwa tayari kumchoma moto ambapo dakika chache tu baadaye askari walifika na kumwokoa.

Kijana huyo aliyekuwa bado hai, aliokolewa na askari  wa doria waliomchukua pamoja na mtu aliyejitaja kama mmiliki wa pikipiki iliyoibiwa.

Crdt: BBC
 
Top