Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (kushoto) akifuta machozi huku akiwa ameshika fomu za kuwania nafasi ya Uenyekiti wa Bazara la Wanawake wa Chadema (Bawacha) alizokabidhiwa na baadhi ya wanakwake makao makuu ya Chama hicho jijini Dar es Salaam  jana.



Kufuatia viongozi wa baraza la Wanawake wa Chadema kujitokeza kwa wingi katika kinyang’anyiro cha kuwania uwenyekiti wa Baraza hilo (BAWACHA) nafasi ambayo kwa sasa inashikiliwa na Suzan Lymo.

Wanachama hao wanaowania nafasi hiyo ni pamoja na Mbunge wa viti maalumu, Chiku Abwao pamoja na Lilian Wasira na Sophia Mwakagenda ambao wao tayari wamekwisha kurejesha fomu zao.

Kufuatia hali hiyo wanawake zaidi ya 30 kutokea Kinondoni, Kawe, Pwani, na Ubungo wamejitokeza siku ya jana majira ya saa tano za asubuhi katika ofisi za Bwawacha na kumchukulia fomu mbunge wa Kawe, Halima Mdee.

Walipotoka katika ofisi hizo za Bwawacha walianza safari ya kumsaka mheshimiwa huyo ili kumkabidhi fomu hiyo. Msafara huwo wa kumsaka Halima Mdee uliokuwa ukiongozwa na mwenyekiti wa wazee kata ya Kunduchi, Elefidena Mali ulikwenda moja kwamoja hadi kwenye ofisi za makao makuu ya Chadema na kufanikiwa kumkuta mheshimiwa huyo.

Walimuomba mbunge huyo kupokea fomu hiyo, na Halima Mdee alikubali kupokea fomu hiyo huku akibubujikwa na machozi. Alitoa shukurani zake na kuwaomba wampe nafasi ya kulifikiria jambo hilo kwa makini halafu atawafahamisha kile ambacho atakifikiria.

Wanawake hao walichangishana pesa kiasi cha shilingi 53,000/ na kumkabidhi mheshimiwa huyo kwaajili ya kulipia gharama za kurejesha fomu hiyo. Ambapo mwisho ni tarehe 30 ya mwezi Agosti.
 
Top