Photo: Panya wamla mtoto Afrika Kusini
http://bbc.in/1vQe6mb 
Mtoto wa mwezi mmoja ameshambuliwa na panya wakati mama yake alipokuwa nje akifua na kumuacha mtoto wake ndani amelala.


Mtoto Erena ambaye amepatwa na masahibu hoyo ya kung’atwa na panya maeneo ya puani na pamoja na vidole vyake vitatu vya mikono huko Alexandra, Johannesburg anasubiri kufanyiwa upasuaji kwaajili ya kurekebishwa maeneo ya uso wake yaliyoathirika.

Mama wa mtoto huyo ambaye alikuwa nje akifua wakati mtoto wake akishambuliwa na panya hao, alisema kuwa aliingia ndani ghafla aliposikia harufu ya damu, na lipofika ndani alimkuta mtoto wake huyo tayari amekwisha jeruhiwa.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kimeeleza kuwa tukio hilo la panya hao waliokuwa na ukubwa usio wa kawaida wamekuwa na kawaida ya kuwauma watoto na wazee katika eneo hilo kulingana na kutokuweka safi mazingira yao
 
Top