Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii Dk. Seif rshid
Bertha Boniphace (25) mkazi wa Kata ya Karoro-Buserere mkoani Geita amefariki dunia katika hospitali ya wilaya ya Geita alipokuwa amelazwa baada na kuugua ugonjwa uliokuwa ukifanana na ugonjwa wa Ebora.



Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kimeeleza kuwa, Bertha Boniphace alikuwa akisumbuliwa na kutapika, kuharisha damu na kutoka damu sehemu za mdomo na puani, dalili ambazo zinashabihiana na zile za ugonjwa wa Ebola hali iliyosababisha watu kufikiria kuwa ameuawa na ugonjwa huo.


Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii imetoa matokeo ya sampuli ziliyopelekwa Nairobi nchini Kenya kuweza kuchunguza chanzo cha kifo cha Bertha Boniface.

Mganga mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Geita, Dk Adam Sijaona alieleza matokeo ya sampuli hizo kuwa yanaonesha Bertha hakuwa na maambukizi ya ugonjwa wa Ebola bali alikuwa anaumwa ugonjwa unaojulikana kitaalamu ‘Chikungunya Viral Hemorrhagic Fever (VHF)


“Bertha hakuuawa na Ebola kama watu wanavyo dhani, bali ni ugonjwa ambao unataka kufanana na Ebola. Huu ni ugonjwa wa Kitropic ambao unaenezwa na mbu aina ya Aedes Aegyti. Aina hii ya mbu ni wachache sana. Na wanapatikana maeneo yenye unyevunyevu” alieleza Dk Sijaona


Mganga mkuu wa mkoa wa Geita, Dk Joseph Kisala naye alieleza kuwa ugonjwa huo ni mpya nchini na haujazoeleka barani Afrika. Pia ugonjwa huo hauna tiba maalumu kama ugonjwa wa Dengue.
 
Top