TUNAOMBA RADHI KWA PICHA ZINAZOTISHA, NI AJALI MBAYA SANA
Zaidi ya Watu 38 wamefariki dunia papo hapo na wengine 86 kujeruhiwa vibaya katika ajali iliyotokea leo asubuhi majia ya saa tano maeneo ya Sabasaba nje kidogo mwa mji wa Musoma.


Ajali hiyo inahusisha Basi la kampuni ya J4 Express lenye nambari za usajiri T 677 CYC lililokuwa likitokea Mwanza kuelekea Silari mkoani Mara, na basi la Kampuni ya Mwanza Coach lenye nambari za usajili T 736 AWJ lililokuwa likitokea Musoma kuelekea Mwanza.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kilichoripoti, chanzo cha ajali hiyo ni basi la kampuni ya J4 kujaribu kulipita gari ndogo Nissan Terano lenye nambari za usajili 332 AKK karibu na daraja ambalo linauwezo wa kupitisha gari moja.

Kutokana na mwendo kasi wa mabasi yote mawili J4 na Mwanza Coach, yalishindwa kupishana na kuvaana uso kwa uso yakijumuisha gari ndogo ambayo ilitumbukia mtoni na kuua watu wawili, mmoja majeruhi.

Majeruhi pamoja na maiti walifikishwa katika hospitali ya mkoa iliyopo Musoma kwaajili ya huduma pamoja na utambuzi kwa wale waliopoteza maisha. Hadi ilipofika majira ya saa kumi na moja jioni idadi ya watu walifariki ilikuwa zaidi ya 40
  
INNALLILLAHI WAINNA ILAIHI RAJIUN – BWANA AMETOA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE
 
Top