UTAMU WA RAHA INAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI
 
Mwili wa mmoja wa majambazi ukiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti

Baada ya UTAMU WA RAHA kuripoti taarifa za ujambazi wa kuteka magari uliofanyika katika tarehe 2 Septemba majira ya saa 2:30 usiku maeneo ya Kilosa njia panda ya Iringa kule Morogoro, watu watano wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wameuawa na jeshi la polisi mkoani Kigoma katika majibizano Yarisasi.


Kamishna msaidizi wa polisi mkoani Humo, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa, Tukio hilo limetokea maeneo ya barabara kuu ya Kasulu Kibondo kwenye pori la Malagalasi majira ya saa 11 alfajiri Septemba 3 mwaka huu.

Askari wa doria walipata taarifa kuwa majambazi kutoka Burundi walikuwa na mpango wa kufanya utekeji wa magari katika eneo hilo. Baada ya askari kupata taarifa hizo walijipanga na kuweka mtego katika eneo la tukio” alisema Kamanda Ibrahim na kuendelea

Baada ya muda majambazi hao walifika eneo la tukio kwa malengo ya kukamilisha mipango yao. Hapo ndipo walipoanza kurushiana risasi na askari polisi.

Jeshi la askari polisi lilifanikiwa kuwaua majambazi watano na kukamata vifaa vilivyokuwa vimekusudiwa kutumiwa katika kufanyia uhalifu huo. Vifaa hivyo ni pamoja na mabomu matatu ya kurusha kwa mkono, silaha za kivita mbili aina ya SMG, pamoja na AK 47, na risasi 64 ” alisema Kamanda Ibrahim.

Miili ya majambazi hao imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Kasulu kwaajili ya Utambulisho.

 
 


 

 
Top