Alisema
kutokana na manispaa hiyo kutokuwa na eneo la wazi, uongozi ulilazimika
kutafuta eneo katika Kijiji cha Kising’a, Tarafa ya Isimani linalomilikiwa na
Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Uyole.
Iringa. Vijana zaidi ya 1,000 kutoka katika
vikundi 36 katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wanatarajiwa kupewa maeneo
ya kilimo na Serikali ili kuwainua kiuchumi.
Ofisa
Kilimo na Mifugo katika halmashauri hiyo, Robert Semaganga alisema hayo hivi
karibuni wakati vijana walipokuwa wakipanda alizeti kwenye mashamba
yaliyotolewa na Serikali.
Semaganga
alisema mpango huo ni utekelezaji wa agizo la Serikali la kutaka kila
halmashauri kutafuta maeneo ya kilimo kwa vijana.
Alisema
kutokana na manispaa hiyo kutokuwa na eneo la wazi, uongozi ulilazimika
kutafuta eneo katika Kijiji cha Kising’a, Tarafa ya Isimani linalomilikiwa na
Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Uyole.
“Tulipoomba
hekta 150 katika kituo hicho, Serikali ya Mkoa ilitoa baraka zote...Lakini
manispaa nayo ilitoa kilogramu 500 za mbegu ya alizeti kwa ajili ya kusaidia
vijana watakaojitokeza kuunda vikundi,” alisema Semaganga.
Alisema:
“Tunamshukuru pia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu kwani
baada ya kupata shamba na mbegu, amejitolea gharama za kulima. Pia leo ametoa
msaada wa usafiri na chakula kwa vijana waliokuja kupanda kwenye shamba hili.
“Mchakato
wa kuwapata vijana umeshafanyika kwa kusajili vikundi viwili kutoka kila kata.”
Msambatavangu
alisema katika mpango huo ametumia zaidi ya Sh3.5 milioni zikiwa ni gharama za
kuandaa shamba la kulima.