Kocha, Zdravko Logarusic akiwapa maelekezo wachezaji wa Simba kabla ya kutimuliwa 

In Summary:


Kabla ya kumtimua Logarusic, uongozi wa klabu hiyo ulipiga hesabu kali. Kocha huyo alichukua Dola 24,000 (Sh 39.7milioni) ambazo ni ada ya kusaini mkataba na ili kuuvunja mkataba anatakiwa alipwe Dola 5,000 (Sh8.1 milioni).
SIMBA ilimpa kocha, Zdravko Logarusic, mkataba wa mwaka mmoja wiki tatu zilizopita. Lakini juzi Jumapili ilifanya uamuzi mgumu kwa kumpiga chini kwa maelezo kwamba haendani na hali halisi ya klabu.

Kabla ya kumtimua Logarusic, uongozi wa klabu hiyo ulipiga hesabu kali. Kocha huyo alichukua Dola 24,000 (Sh 39.7milioni) ambazo ni ada ya kusaini mkataba na ili kuuvunja mkataba anatakiwa alipwe Dola 5,000 (Sh8.1 milioni).

Viongozi hao wakaona ni bora kupoteza Sh 47.8 milioni kuliko kuangamiza kiasi cha Sh3 bilioni na kuambulia patupu kwenye Ligi Kuu Bara msimu ujao.
Simba imepanga kutumia bilioni hizo msimu ujao, ni fedha nyingi, zinawauma viongozi wa klabu hiyo na ni dhahiri kuwa wanataka timu yao ifanye vizuri baada ya kutumia fedha hizo na si kitu kingine. Tathmini hiyo ya hesabu ilionyesha kuwa kocha Logarusic haendani na kasi yao, makosa yake yamekuwa ni yale yale siku zote na amekuwa habadiliki. Wachezaji wanaonekana kumchoka hivyo kuokoa jahazi, wakafanya maamuzi magumu.

Mwanaspoti ambayo ilikuwa ikifuatilia nyendo za kocha huyo kwa karibu tangu ajiunge na klabu hiyo inakuletea sababu 10 zilizomwonyesha mlango wa kutokea;

Ukali uliopitiliza
Ukiwa katika uongozi sehemu yoyote unahitaji kuwa mkali kwa baadhi ya mambo, lakini usisahau kutumia busara.
Logarusic alikuwa mkali, busara kwake ni kitu cha mwisho, mchezaji akikosea kidogo alikua akijuta. Ukali wake ulipitiliza hadi baadhi ya wachezaji waliogopa. Hali hiyo iliwachosha viongozi waliokuwa wakimwomba apunguze, japo hakuwasikiliza.

Kulazimisha mambo
Kocha Logarusic anaiamini akili yake kwa asilimia 100, ana amini kila akifanyacho ni sahihi, ni mgumu kutekeleza maoni ya wengine. Imani hiyo ilimfanya awe na tabia ya kulazimisha mambo. Tabia hiyo ilimfanya Loga kuwatema wachezaji 12 kwenye kikosi chake, ni idadi kubwa ya wachezaji lakini alilazimisha hadi yakatimia, Uhuru Selemani pekee ndiye aliyesalimika tena kwa jitihada zake mwenyewe na za baadhi ya viongozi. Uongozi ukaona kuburuzwa.

Wachezaji wa Mbeya City
Kabla ya kwenda mapumzikoni kwao Croatia, Logarusic alipendekeza klabu hiyo isajili wachezaji kadhaa kutoka Mbeya City wakiwamo Deus Kaseke, Saady Kipanga na Anthony Matogolo. Aliporejea hakumkuta hata mmoja wao kikosini hapo, akaanzisha varangati akitaka wasajiliwe.
 
Top