https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhFspxv2WCMTb5na7FTm3gjuF692EyC8QLMHmCD5UMGxfdd2jcYuMKdeq8xfqPwjGDwXyhX5SmYQch5tULzKypGPR12nJ0_bHG-lC2ZWCZO1LlESoHhloaUqlm1Fu_JR159rkq-86EXOtju/s1600/img_3286.jpg                   
Wakulima wa zao la Pamba wa Simiyu katika wilaya ya Bunda mkoani Mara, wamejikuta wakipigwa changa  la macho baada ya kupeleka mazao yao ya pamba sokoni kwa lengo la kuuza.


Mtu mmoja ambaye aliyetambulika kuwa ni karani, alishiriki kuwaingiza mjini wananchi hao (wakulima) kwa kununua pamba zao na kuwalipa kwa pesa za bandia.

Baada ya wakulima hao kubaini utapeli wa mtu huyo, taarifa zilifikishwa kwenye vyombo vya sheria ambako walimfuatilia mtuhumiwa na kumtia mbaroni. Pesa hizo zilipokusanywa na wakulima hao zilipatikana noti ambazo kama zingekuwa halali zingekuwa na thamani ya shilingi 200,00/=

Mtuhumiwa ameshikiliwa na jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi ili kama akipatikana na hatia kuweza kuleta fundisho kwa watu wengine ambao wanajihusisha na biashara haramu kama hiyo.

 
Top