Kufuatia utafiti ambao umefanywa na chama cha wanawake wanasheria (WLAC) mnamo mwaka 2012/2013 katika mikoa ya Kusini, imegundulika kuwa asilimia 80 ya ndoa 100 zina matatizo na zinakabiliana na migogoro ya mara kwa mara.


Kwa mujibu wa kaimu mkurugenzi wa WLAC Jane Magigita anasema kuwa utafiti huwo ambao umefanyika mikoa ya Kusini kwa lengo la kubaini chanzo cha kuvunjika kwa ndoa nyingi hasa katika maeneo hayo.

Anasema kuwa katika mashauri 20 ya ndoa ambayo huwasilishwa kila siku kwenye ofisi za ustawi wa jamii, ni ndoa 5 tu ambazo hufanikiwa kusuluhishwa na kurejeshwa katika hali ya kawaida.

Kwa mujibu wa Magigita ameeleza kuwa sababu kadhaa ambazo zimekuwa zikipelekea ndoa nyingi kuvunjika ni pamoja na vitendo vya kikatili ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia. Kwa mfano kupigwa mbele ya watoto, kuvuliwa nguo hadharani na matusi ya kudhalilisha.

Stela Stephene ambaye ni Afisa ustawi wa jamii katika wila ya Lindi, amesema kuwa kesi nyingi huishia kusuluhishwa katika ngazi ya familia, na chache ndizo hupelekwa katika ngazi za juu.

Itaendelea kesho..... 

 
Top