Kocha Mbrazil Marcio Maximo, amesema kuwa ameamua kuja na mbinu mpya ya kuiboresha timu yake anayoifundisha ili iweze kuimarika na kuwa na kiwango cha juu zaidi



Kocha huyo ambaye alishawahi kuifundisha timu ya Taifa Stars, amesema kuwa kwa kutumia mbinu hiyo timu yake anayoifundisha itakuwa bora na bora zaidi katika msimu wa ligi guu.

Alisema kuwa katika mazoezi ya kukinoa kikosi hicho kwaajili ya maandalizi ya ligi kuu, atahakikisha kila mchezaji katika kikosi cha timu hiyo anakuwa na uwezo wa kuchezea nafasi tatu tofauti pasipo kutetereka. 

Kitendo hicho kitasaidi hata ikitokea mchezaji mmoja akawa anaumwa ama ameshindwa kufika kwenye mechi kwa sababu zisizozuilika, haitakuwa kikwazo mtu mwingine kuziba pengo lake.

“Ninataka soka la Kibrazili Yanga, kwa kuanza ninataka kila mchezaji awe na uwezo wa kucheza nafasi tatu hadi nne.

“Hiyo itanisaidia mimi kama siku moja ikitokea mmoja majeruhi au ana kadi nyekundu basi mwingine anachukua nafasi yake, pia itanisaidia kuleta changamoto ya namba kwenye timu,” alisema Maximo 

Jiunge hapa na Group letu la Facebook tuzungumzie kuhusu Soka>> 

 
Top