Lango la kuingilia hospitali ya Temeke ambapo mgonjwa anayedaiwa kuwa na ugonjwa wa ebora kulazwa.

Kwa ufupi 
Msichana mmoja mwenye umri wa miaka 14 jijini Dar, amelazwa hospitali ya Temeke huku akiwa na dalili zote za kuwa na ugonjwa wa Ebora.


Kwa mujibu wa taarifa za mganga mfawidhi wa hospitali ya Temeke Dr. Amani Malima amethibitisha kuwepo kwa msichana huyo hospitalini hapo. 

Msichana huyo ambaye aliingia nchini jana akitokea Benin, Afrika Magharibi alionekana kuwa na dalili za ugonjwa huwo. Kwani baada ya kuhojiwa na madaktari alisema kuwa anahisi maumivu makali ya viungo, miguu na mikono alieleza Dr.Amani.

Mganga huyo ameendelea kutoa maelezo yake kwa kusema kuwa baada ya kumfanyia vipimo msichana huyo alibainika kuwa na malaria, lakini vipimo vya ebora bado havijatoa majibu ambapo majibu yake yatatoka leo. Aliongeza kuwa endapo msichana huyo hata gundulika na maambukizi ya ugonjwa huwo watamruhusu.

 
Top